Saturday, December 1, 2012
Dumu Sports: MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL
Dumu Sports: MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL: Mesut Ozil katika moja ya mechi za timu yake ya Real Madrid MANCHESTER , Uingereza Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson atu...
MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL
![]() |
| Mesut Ozil katika moja ya mechi za timu yake ya Real Madrid |
MANCHESTER, Uingereza
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson atupia jicho lake kwa
kiungo wa Real Madrid Mesut Ozil, 24. Mchezaji huyo raia wa Ujerumani amekuwa
sio chaguo la kwanza la meneja wa Real Madrid Mreno Jose Maurinho tokea
kuwasili kwa Luka Modric toka Tottenham Hotspurs ya Uingereza.
![]() |
| Mesut Ozil akiichezea ujerumani katikaMashindano ya UEFA |
Sir Alex Ferguson anamtaka Ozil kwa udi na uvumba aje kuchukua nafasi ya
kiungo mkongwe wa timu hiyo Paul schools, 38. Kwa sasa Scholes anaonekana
dhahiri kuchoka na huenda akatangaza kustaafu soka kwa mara ya pili mwishoni
mwa msimu huu.
Kwa upande wa Ozil ameonekana hana furaha kwa kutokuwa chaguo la kwanza
kwenye klabu yake. Mesut Ozil alijiunga na Real Madrid miaka miwili iliyopita
akitokea timu ya Werder Bremen ya Ujerumani kwa ada ya pauni 12 milioni na
amekuwa akipokea mshahara wa pauni 110,000 kwa wiki ambazo kwa timu kama
Manchester United ni mshahara wa kawaida. Wataalam na wachambuzi wa soka
wanatabiri kama Real Madrid itaamua kumuuza Ozil itamuuza kwa ada isiyopungua
pauni 24 milioni.
Dumu Sports: LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL...
Dumu Sports: LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL...: Uingereza, Mshambuliaji wa timu ya Liverpool Luis Suarez ameshinda Barclays Golden Boot baada ya kuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufik...
LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL AWARD
Uingereza,
Mshambuliaji wa timu ya Liverpool Luis Suarez ameshinda Barclays Golden Boot baada ya kuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufikisha mabao kumi. Suarez amefikisha mabao hayo katika michezo 13 aliyoichezea timu yake ya Liverpool msimu huu.
Akiongea baada ya kupokea zawadi hiyo, Suarez alimshukuru meneja wake
Brendan Rodgers kwa kumchochea kuongeza juhudi sio kwake yeye tu bali kwa kila
mchezaji wa timu ya Liverpool. Pia alisema meneja wake anamchezesha kwa staili
anayoipenda kwa kumfanya kuwa mshambuliaji huru na pekee kwenye kikosi sanjari
na kumtia moyo kwamba atafunga mabao kitu ambacho kimemuongezea kujiamini.
Pia aliwapongeza viungo washambuliaji vijana wa timu hiyo Raheem
Sterling na Suso kwa viwango vyao na jinsi wanavyojifunza toka kwa wachezaji
wazoefu kama Steven Gerrard, Pepe Reina na Jamie Carragher na watakuja
kufanikiwa sana siku za baadae.
Subscribe to:
Comments (Atom)





