![]() |
| Mesut Ozil katika moja ya mechi za timu yake ya Real Madrid |
MANCHESTER, Uingereza
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson atupia jicho lake kwa
kiungo wa Real Madrid Mesut Ozil, 24. Mchezaji huyo raia wa Ujerumani amekuwa
sio chaguo la kwanza la meneja wa Real Madrid Mreno Jose Maurinho tokea
kuwasili kwa Luka Modric toka Tottenham Hotspurs ya Uingereza.
![]() |
| Mesut Ozil akiichezea ujerumani katikaMashindano ya UEFA |
Sir Alex Ferguson anamtaka Ozil kwa udi na uvumba aje kuchukua nafasi ya
kiungo mkongwe wa timu hiyo Paul schools, 38. Kwa sasa Scholes anaonekana
dhahiri kuchoka na huenda akatangaza kustaafu soka kwa mara ya pili mwishoni
mwa msimu huu.
Kwa upande wa Ozil ameonekana hana furaha kwa kutokuwa chaguo la kwanza
kwenye klabu yake. Mesut Ozil alijiunga na Real Madrid miaka miwili iliyopita
akitokea timu ya Werder Bremen ya Ujerumani kwa ada ya pauni 12 milioni na
amekuwa akipokea mshahara wa pauni 110,000 kwa wiki ambazo kwa timu kama
Manchester United ni mshahara wa kawaida. Wataalam na wachambuzi wa soka
wanatabiri kama Real Madrid itaamua kumuuza Ozil itamuuza kwa ada isiyopungua
pauni 24 milioni.



No comments:
Post a Comment