Tuesday, December 2, 2014

WENGER AWAPONDA WANAOTAKA AACHIE NGAZI

Mashabiki wa Arsenal waliochoshwa na matokeo ya klabu yao

London,
Kocha wa timu ya Arsenal mfaransa Arsene Wenger amepinga vikali na kuwabeza wale wanaosema uwezo wake kuongoza kikosi cha timu ya Arsenal umeshuka. Akiongea juu ya bango la tambala lililokuwa likipitishwa na mashabiki wa timu hiyo katika mchezo kati ya timu hiyo na West Bromwich Albion jumamosi iliyopita. Bongo hilo liliandikwa Arsene tunakushukuru kwa kututengenezea kumbukumbu nzuri, lakini umefika wakati wa kutuaga /ujiuzuru (ARSENE THANKS FOR THE MEMORIES BUT IT’S TIME TO SAY GOODBYE).

Arsene Wenger
Kama lilivyosema bango hilo, Wenger alitumia rekodi yake ya mafanikio kuwaponda wale wanaomtaka ajiuzulu. Wanger alisema ameiingiza kwenye 16 bora za Uefa Champions League kwa miaka 15 mfululizo, rekodi ambayo hakuna Klabu iliyoweza kuifikia. Wenger aliendelea kuwaponda wale wanaomwona hana uwezo wa kufundisha klabu kubwa, kwamba amekuwa mwalimu wa klabu mbalimbali kubwa Barani Ulaya tangu mwaka 1983, na kama kuna mtu anadhani hana uwezo basi yeye (Wenger) ni genius kwa kuweza kuficha mapungufu hayo yasionekane kwa muda wote huo.

Shutuma kwa Arsene Wenger zinakuja kutokana na klabu hiyo kutopata vikombe kwa siku za karibuni.  Kwa sasa Arsenal inashika nafasi ya 6 katika msimamo wa ligi kuu ya Uingereza.

Friday, November 14, 2014

TWITE AGOMA KUONGEZA MKATABA YANGA

Twite wakati akisaini mkataba uliopita
Mashabiki wa Yanga wakimkejeli
aliyekuwa Mwenyekiti wa Simba
kwa kushindwa kumsajili Twite siku
Twite aliposaini Yanga
Shabiki wa Yanga akijongea uwanjani
Beki mkabaji wa Yanga Mbuyu Twite amegoma kuongeza mkataba mpya na mabigwa hao wa zamani wa VPL. Habari ambazo sio rasmi toka ndani ya klabu hiyo zinasema mchezaji huyo bado anaidai klabu hiyo ya mtaa wa Jangwani na Twiga fedha (signing fee) ya usajili  uliopita ambazo baso hajamaliziwa. Kwa sasa Twite anawindwa na klabu za Simba SC na Azam FC zote za Dar es salaam.







GARI BOVU LA SIMBA LASHIKA KASI MTEREMKONI

Kocha wa Simba Patrick Phiri
Kocha mkuu wa Simba Sports Club, Mzambia Patrick Phiri amewashukuru mashabiki na wapenzi wa timu hiyo kwa kuipa sapoti klabu kuwatia nguvu wachezaji kulikowapa hamasa ya kupata ushindi wa kwanza katika msimu huu wa VPL. Akiongea kwa furaha; Phiri amejinasibu kwamba huu ni mwisho wa matokeo ya sare kwa klabu hiyo ambayo imekuwa ikiyapata katika mechi sita za kwanza mfululizo tangu kuanzakwa msimu huu wa VPL.
"Nawashukuru  sana viongozi, wachezaji, pamoja na mashabiki wetu ambao wametupa sapoti hadi kufanikiwa kupata ushindi. Haikuwa rahisi na kwa sasa nasema rasmi kuwa matokeo ya sare baibai kinachofuata ni ushindi kwa kila mechi"
Hadi sasa Simba ina pointi tisa ikiwa nyuma kwa pointi tisa toka kwa vinara wa ligi hiyo ambapo Mzambia huyo bado anaamini timu hiyo itafanya vizuri na hata kuchukua ubingwa msimu huu.

WAWA ATUA AZAM FC

Mwenyekiti wa klabu ya Azam FC Sheikh Said Muhammed kushoto akimkabidhi jezi Wawa (Picha  
kama ilivyo katika mtandao wa klabu hiyo) 
Klabu ya soka ya Azam FC imekamilisha usajili wa beki Sergio Wawa kutoka Elmeirreickh ya Sudan. Raia huyo wa Senegal anakuja kuongeza nguvu katika ukuta imara wa mabingwa hao watetezi wa Vodacom Premier League (VPL) wanaonolewa na Mcameroon Joseph Omog  ambaye itamlazimu kupunguza mcehezaji mmoja wa kimataifa katika kikosi chake kuruhusu Wawa kucheza.
Wawa (wakati akiwa El Merreickh) akimkaba Thiago wa Buyern Muenchen timu hizo zilipopambana katika mchezo wa kirafiki kwenye uwanja wa Al Saadjijini DOHA Qatar mapema mwezi januari mwaka huu (Picha na mtandao wa Get Image)

Sunday, August 18, 2013

KANYE WEST, KIM NA MTOTO WAO NORTH WEST WAONEKANA HADHARANI JUMATANO KWA MARA YA KWANZA

California,
Baada ya kuepuka paparazzi paparazzi wote majira ya joto waliokuwa kikwazo kwake "kujitokeza hadharani" katika video mbili akionesha tu uso wake, Kim Kardashian hatimaye ajitokeza hadharani siku ya Jumatano.
Na yeye hakuwa peke yake-Kanye West na mtoto wao wa miezi 2 , North West, walikuwa pamoja naye. watatu hawa hawakuwahi kupiga picha ya pamoja tangu kuzaliwa kwa North mnamo Juni 15.

RATIBA NA MATOKEO YA LIGI KUU YA UINGEREZA

Barclays Premier League
Ratiba na Matokeo ya Wiki ya Kwanza 
Muda  (saa) wa Tanzania
Jumamosi, Agosti 17 2013
Liverpool
1

Stoke City
0
West Ham
2

Cardiff City
0
Sunderland
0

Fulham
1
Norwich City
2

Everton
2
West Brom
0

Southampton
1
Arsenal
1

Aston Villa
3
Swansea City
1

Man United
4
Jumapili, Agosti 18 2013
Crystal Palace
3:30 PM
Tottenham
Chelsea
6:00 PM
Hull City Tigers
Jumatatu, Agosti 19 2013
Man City
10:00 PM
Newcastle

Saturday, August 17, 2013

RAZ-B WA B2K APIGWA CHUPA YA KWENYE SHOO CHINA, APOTEZA FAHAMU

China,
Raz-B baada ya kushambuliwa na chupa.
Mwanamuziki wa zamani wa kundi la B2K, Raz-B amelazwa hospitali nchini China baada ya kupigwa chupa na mlinzi wake (mshikaji). Hali yake imebadilika leo na amepoteza fahamu. Raz-B(28) alikuwa akipiga shoo katika klabu ya usiku na ghafla kulitokea mapigano upande wa mashabiki wakipigana ngumi, na alipojaribu kutuliza hali ghafla alikumbana na maswaibu hayo. 

Chupa aliyopigwa nayo ilimtoboa tundu refu kwenye mdomo na alisikika akilalamikia maumivu makali. Raz-B pia alishukuru kwa kuwahishwa hospitali. Alisema:

"F**k this s**t hurts. I have a f**king hole in my lip. Thank God I made it to the hospital"
Raz-B
Jana, aliruhusiwa baada ya kushonwa nyuzi kazaa mdomoni, lakini alishindwa kuamka asubuhi ya leo ambapo wacheza shoo wake walimuwahisha hospitali haraka. Raz-B aliwahi ku-hit akiwa na kundi la B2K kipindi hicho akiwa na Omarion, Lil' Fizz, na J-Boog wakiwa na ngoma zao kali kama "Bump Bump Bump", "Why I love you", na "Girlfriend".
Chanzo: TMZ