Friday, November 30, 2012

ADIOS HECTOR "MACHO" CAMACHO

Mama wa marehemu Hector "Macho" Camacho, Maria Matias
akilia "wamemuua, wamuuaa" wakati akitoa heshima ya mwisho 

SAN JUAN, Puerto Rico

Mabondia, wapenzi wa ngumi, na wanandugu wa bondia Hector “Macho” juzi (jumanne) kuuaga na kuuzika mwili wa mwanamasumbwi nguli. Waombolezaji waliobeba picha mbalimbali za Macho walipita mbele ya jeneza lake kumuaga marehemu.

waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu
Hector "Macho" Camacho
Wakiongozwa na familia ya marehemu wakiongozwa na mama wa marehemu Maria Matia walitoa heshima za mwisho. Camacho aliuawa tarehe 20 Novemba akiwa kwenye maegesho ya magari ya bar moja katika mji wa Bayamon nchini Purto Rico. Katika tukio hilo rafiki yake wa karibu alifariki papo hapo na Camacho alifariki siku tatu baadaye akiwa kwenye matibabu.

Hadi sasa polisi nchini humo wanasema wana orodha ya washukiwa lakini bado hawajawatia mbaroni.

No comments:

Post a Comment