![]() |
| Mama wa marehemu Hector "Macho" Camacho, Maria Matias akilia "wamemuua, wamuuaa" wakati akitoa heshima ya mwisho |
SAN JUAN, Puerto Rico
Mabondia, wapenzi wa
ngumi, na wanandugu wa bondia Hector “Macho” juzi (jumanne) kuuaga na kuuzika
mwili wa mwanamasumbwi nguli. Waombolezaji waliobeba picha mbalimbali za Macho
walipita mbele ya jeneza lake kumuaga marehemu.
![]() |
| waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu Hector "Macho" Camacho |
Wakiongozwa na familia ya
marehemu wakiongozwa na mama wa marehemu Maria Matia walitoa heshima za mwisho.
Camacho aliuawa tarehe 20 Novemba akiwa kwenye maegesho ya magari ya bar moja
katika mji wa Bayamon nchini Purto Rico. Katika tukio hilo rafiki yake wa
karibu alifariki papo hapo na Camacho alifariki siku tatu baadaye akiwa kwenye
matibabu.
Hadi sasa polisi nchini
humo wanasema wana orodha ya washukiwa lakini bado hawajawatia mbaroni.


No comments:
Post a Comment