Thursday, November 22, 2012

ROBERTO DI MATTEO APIGWA CHINI

Roberto Di Matteo akifuatilia moja ya
michezo alipokuwa kocha wa Chelsea

Chelsea imetangaza kumtema maeneja wake Mtaliano Roberto Di Matteo kwa kilichoelezwa kutokuonesha mwenendo mzuri wa timu. Di Matteo mabaye katika uongozi wake klabuni hapo aliingoza Chelsea maarufu kama “The Blues”michezo 42 ambapo ilishinda 24, kupoteza 9 na kutoka sare 9. Kufutwa kazi kwa Di Matteo's kulitazamiwa kufuatia klabu hiyo ya London kupoteza kwa mabao 3-0 dhidi ya Juventus na kuifanya kuwa bingwa mtetezi wa kwanza kutolewa katika hatua ya makundi katika historia ya mashindano ya klabu bingwa barani ulaya (UEFA Champions League).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotelewa na mtandao wa klabu www.chelseafc.com, klabu hiyo yenye uwanja wake Stanford Bridge imethibitisha kuondoka kwa Di Matteo. Sehemu ya taarifa ilisema Chelsea imevunja mkataba na na meneja Roberto Di Matteo. Kiwango cha mchezo na matokeo ya timu kwa siku za karibuni yamekuwa hayaridhishi na mmiliki na bodi wameona mabadiliko ni lazima yafanyike sasa kuiwezesha klabu kuelekea kwenye mwelekeo sahihi kwa kuwa ikielekea kwenye kipindi muhimu zaidi cha msimu.
Roberto Di Matteo akisherehekea ubingwa wa UEFA
Champions League na wapenzi wa Chelsea jijini London

Klabu hiyo ilikumbana na wakati mgumu wakati ikitafuta nafasi ya kuingia katika hatua ya makundi za ligi ya mabingwa huku ikiendelea kupigana kubakia katika nafasi za juu katika ligi ya nyumbani. Lengo la klabu ni kubakia katika nafasi ya kiushandani zaidi katika mashindano yote ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Roberto Di Matteo alipokuwa mchezaji wa Chelsea
Pia klabu hiyo imemshukuru meneja huyokwa yote mazuri aliyoifanyia klabu hiyo kubwa hasa likiwa ni kuiwezesha kuchukua ubingwa katika ligi ya klabu bingwa barani ulaya sanjari na kuipa ushindi wa kombe la chama cha soka cha Uingereza (FA Cup). Klabu hiyo inasema haitaweza kumsahau Muitaliano huyo kwa mchango wake mkubwa alioutoa ambao ni wa kihistoria katika klabu hiyo na imesema iko tayari kumkaribisha muda wowote ule.
Wakati huohuo klabu hiyo ikitazamiwa  kumtangaza kocha mpya wa klabu hiyo baada ya kumfukuza kazi Di Matteo, kumekuwa na kundi linalomlaumu Di Matteo kwa matokeo mabaya katika michezo ya hivi karibuni. Katika michezo nane ya mwisho aliwaongoza wazee wa ‘darajani’ kushinda michezo ,miwili tu kitu kilichomplekea mmiliki wa klabu hiyo asiye mvumilivu Roman Abramovich kumfukuza kazi.

No comments:

Post a Comment