Wednesday, November 14, 2012

Harambee Stars Yatua Mwanza

Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Paulsen

Harambee Stars ya Kenya jana iliwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza tayari kwa mchezo wake wa leo dhidi ya Taifa Stars. Kocha mkuu wa Wakenya hao Henri Michel amejinadi kuwa atatumia kikosi kilekile kilichoisumbua Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Oktoba 16 katika uwanja wa Nyayo. Katika mchezo huo Afrika Kusini ilipata ushindi mwembamba wa mabao 2-1.

Harambee Stars imewasili bila ya kipa wake namba moja Arnold Origi aneyekipiga katika timu ya Ullkisa amabaye amebanwa na ratiba ngumu ya ligi. Pia Wakenya hao watamkosa mshambuliaji wao hatari Victor Wanyama ambaye anakabiliwa na majeruhi. Michel amemuita Jactone Odhiambo wa Ulinzi kuziba pengo la Origin a Anthony Akumu wa Gor Mahia kuziba pengo la Wanyama.

Naye kocha wa Taifa Stars Kim Paulsen amefanya mabadiliko kidogo kwenye kikosi chake kwa kuwaacha Said Bahanuzi (Yanga) na Haruna Moshi “Boban” (Simba). Paulsen ameongeza kiungo hatari Amri Kiemba (Simba) pamoja na damu changa kama Frank Domayo (Yanga), Simon Msuva (Yanga), Christopher Edward (Simba). Pia katika kikosi hicho hakuwaacha wachezaji wenye asili ya visiwani ambao wataruhusiwa kujiunga na Zanzibar Heroes mara tu baada ya mchezo wa Leo. Wachezaji hao ni Aggrey Morris, Said Nassor “Cholo”, na Issa Rashid.

No comments:

Post a Comment