Friday, November 9, 2012

Wenger Alegeza Msimamamo Wake

Jack Wilshere
Meneja wa washika bunduki wa London Mfaransa Arsene Wenger amelegeza msimamo wake na kumrushusu mchezejai wake Jack Wilshere (20) kuchezea timu ya taifa ya Uingereza itakapopambana na Sweden wiki ijayo. Awali Wenger alimtaka kocha wa Uingereza Roy Hogson kumpumzisha mchezaji huyo kwa kuwa alikuwa majeruhi kwa muda mrefu. Mameneja hao walifikia muafaka wa kumruhusu Wilshere mara baada ya mchezo kati ya Arsenal na Manchester United ambapo Wilshere alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Akiongea na skysports.com Wenger alisema "Ninaona ni mapema mno kwa Jack lakini nimeongea na Roy Hodgson kwa simu na tumeelewana na kufikia muafaka mzuri”
 "Kizuri zaidi ni kuwa hatacheza mwishoni mwa wiki hii kwa kuwa na adhabu ya kadi nyekundu hivyo atapumzika na kujiunga na kikosi kama Roy anavyotaka”

No comments:

Post a Comment