![]() |
| Jack Wilshere |
Meneja wa washika
bunduki wa London Mfaransa Arsene Wenger amelegeza msimamo wake na kumrushusu mchezejai
wake Jack Wilshere (20) kuchezea timu ya taifa ya Uingereza itakapopambana na
Sweden wiki ijayo. Awali
Wenger alimtaka kocha wa Uingereza Roy Hogson kumpumzisha mchezaji huyo kwa
kuwa alikuwa majeruhi kwa muda mrefu. Mameneja hao walifikia muafaka wa kumruhusu
Wilshere mara baada ya mchezo kati ya Arsenal na Manchester United ambapo
Wilshere alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Akiongea na skysports.com Wenger alisema "Ninaona ni mapema mno kwa Jack
lakini nimeongea na Roy Hodgson kwa simu na tumeelewana na kufikia muafaka
mzuri”
"Kizuri zaidi ni kuwa hatacheza mwishoni
mwa wiki hii kwa kuwa na adhabu ya kadi nyekundu hivyo atapumzika na kujiunga
na kikosi kama Roy anavyotaka”

No comments:
Post a Comment