Monday, November 26, 2012

'MACHO' CAMACHO AFARIKI DUNIA


SAN JUAN, Puerto Rico
Hector 'Macho' Camacho katikati akiwa na warembo
Amy Camacho mke wa Hector 'Macho' Camacho
Hector ''Macho'' Camacho katika uhai wake alikuwa ni bondia anayejituma na kujiamini mwenye ngumi nzito na mtindo wa kujituma katika mapambano yake na mtukutu nje ya uwanja. Hector ‘Macho’ Camacho alikutwa amefariki siku ya jumamosi baada ya kuvamiwa katika sehemu ya kuegeshea magari katika mji wa Bayamon huko Puerto Rico ambako ndiko alikozaliwa. Polisi walikuta pakti za madawa ya kulevya aina ya cocaine katika gari alilokuwemo.
Camacho, amefariki akiwa na umri wa miaka 50, atakumbukwa kwa uwezo wake mkubwa wa kuburudisha na kupendwa na mashabiki ambapo walikuwa wakimpokea kwa kibwagizo ''It's Macho time!'' kabla hajapanda ulingoni. Camacho alikuwa na kipaji na mbinu zilizowatisha na wapinzani wake na kumfanya kuwa bondia wa kiwango cha juu katika kipindi hicho.
Enzi za ujana wake

Macho akipelekwa hospitali
Macho alipigana kwa kipindi cha miongo mitatu tokaea pambano lake la kwanza dhidi ya David Brown jijini New York mwaka 1980 hadi pambano lake dhidi ya Saul Duran huko Kissimmee, Florida, mwaka 2010. Katika uhai wake alipambana na mabondia nyota mbalimbali wakiwamo Sugar Ray Leonard, Felix Trinidad, Oscar De La Hoya, Roberto Duran na wengineo wengi.

No comments:

Post a Comment