Wednesday, November 14, 2012

THE CRANES KUIVAA HARAMBEE STARS

Timu ya taifa ya Kenya "Harambee Stars"

Timu ya soka ya Uganda The Cranes itashuka dimbani kuikaribisha timu ya taifa ya Kenya almaarufu Harambee Stars. Timu hizi zitachuana katika mchezo wa ufunguzi wa michuano ya CECAFA Challenge Cup mchezo utakaochezwa tarehe 24 Novemba mwaka huu jijini Kampala.

Timu ya taifa ya Uganda "The Cranes"
The cranes bado wana uchungu wa kubaniwa na Harambee Stars nafasi ya kushiriki michuano ya mataifa ya Afrika. Katika mchezo huo Wakenya hao waliilazimisha The Cranes sare isiyo na magoli (suluhu), mchezo huo ulifanyika huko Namboole. The Cranes pia katika mchezo wake wa mwisho ilifungwa kwa penati 8-9 na Zambia hapohapo Namboole mwezi Januari mwaka huu.

Kabla ya mechi hiyo ya ufunguzi timu za Ethiopia na Sudani Kusini zitapambana katika mchezo unaotazamiwa kuanza majiara ya saa tisa (9) alasiri kwa saa za Afrika Mashariki. Kwa sasa Uganda ipo katika nafasi ya 88 na Kenya ipo katika nafasi ya 130 ya ubora wa viwango vya soka duniani.

No comments:

Post a Comment