Tuesday, November 27, 2012

RICKY HATTON ASTAAFU BAADA YA KUPIGWA TENA

Manchester
Sir Richard 'Ricky' Hatton

Bondia Mwingereza Ricky Hatton (34) ametangaza kustaafu tena kwa mara ya pili baada ya jaribio lake la kurudi tena kwenye masumbwi kushindwa. Katika pambano lake la kurudi kwenye mchezo huu aliambulia kichapo kikali alipopigwa kwa ‘knockout’ na Vyacheslav Senchenko wa Ukraini jijini Manchester Uingereza jumamosi iliyopita.

Mashabiki wapatao 20,000 walijitokeza kuja kushuhudia kurudi kwa bingwa huyo wa zamani wa dunia katika mji wake wa nyumbani. Ricky alianza pambano hilo vizuri lakini alionekana kuchoka kadri muda ulivyokuwa ukisonga mbele na kumpa nafasi Senchenko (35) kumtupia makonde makali. Ricky alilamba mchanga na alipohesabiwa alishindwa kuinuka na kumfanya mwamuzi kumpa ushindi Senchenko. Senchenko ameendelea kuboresha rekodi yake ambapo hadi sasa amepoteza pambano moja (1)tu kati ya thelasini na nne (34) aliyocheza.
Sir Richard Hatton  akionesha moja ya mikanda yake

Sir Richard 'Ricky' Hatton akiaga mashabiki alipotangaza kustaafu kwa mara ya pili
Akiongea baada ya pambano Hatton alisema"nilitaka walau pambano moja zaidi kuona kama naweza kurejea, na nimeona sintoweza, nimeona sina uwezo tena.” "Nimejiangalia kwenye kioo na nikajiambia mwenyewe nimejitahidi, na sijilaumu”.

No comments:

Post a Comment