![]() |
| Kocha wa Man City Roberto Mancini |
Mabingwa
wa Uingereza Manchester City jana waliaga rasmi michuano ya klabu bingwa barani
ulaya kwa mara ya pili mfululizo. Bao la mapema la Mfaransa Karima Benzema
aliloifungia timu yake ya Real Madrid ya Hispania liliweza kuikatisha ndoto ya
Man City kuingia hatua ya 16 bora ya michuano hiyo. Katika mchezo huo timu hizo
zilitoka sare ya bao 1-1 bao lakusawazisha la Man City likifungwa Sergio Kun
Aguero kwa njia ya penati dakika 15 kabla ya mchezo kumalizika baada ya
kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari na Alvaro Alberoa ambaye alitolewa
kwa kadi nyekundu.
![]() |
| Kocha wa Arsenal Arsene Wenger |
Wakati huo huo Arsenal ilikata tiketi yake kwenye hatua ya 16 bora
baada ya kuwafunga mabingwa wa Ufaransa Montpellier kwa mabao 2-0. Mabao hayo
yalifungwa na Jack wilshere na Lukas Podolski.


No comments:
Post a Comment