Lionel
Messi ameilaumu timu yake pale iliposhtukizwa na kichapo cha mabao 2-1 wakati
ilipochuana nan timu ya Celtic ya Uskochi katika mpambano wa Ligi ya Mabingwa
ya Ulaya maarufa kama UEFA Champions League. Mchezaji huyo nguli wa timu ya
Barcelona amelaumu umaliaziaji mbovu pale timu yake ilipokuwa ikilisogelea
lango la wapinzani wao na kupelekea vigogo hao wa soka wa Hispania na kupoteza
mchezo wa hatua ya makundi kwa mara ya kwanza katika miaka kipindi cha mika
mitatu.
Messi anakiri kuwa pamoja na Barcelona's
kuonesha kiwango bora cha mchezo wa jana ikiwa ugenini kulinganisha na mchezo
wa kwanza timu hizo zilipokutana katika dimba la Camp Nou (nyumbani Barcelona)
ilipopata ushindi wa mabao mawili kwa moja; bado vinara hao wa ligi ya kuu ya
soka ya Hispania walipoteza nafasi nyingi kupitia kwa Messi mwenyewe, Sanchez,
Xavi, naIniesta. Katika mchezo huo washambualiaji Lionel Messi na Alexis
Sanchez kila mmoja aligonga mwamba mara moja huku kipa namba tatu wa zamani wa
Newcastle United akiokoa michomo mingi iliyokuwa ikielekezwa katika lango la
Celtic. Katika mchezo huo Scotland Celtic ilianza kufumania nyavu za wapinzani
wao kupitia kwa mshambuliaji wao Mkenya Victor Wanyama na baadae kuongeza bao
la pili kupitia kwa Tony Watt kabla ya Lionel Messi kuipatia Barca bao la
kufutia machozi huku muda ukiwa umeyoyoma.
Messi amesema Celtic katika michezo
yote miwili wameonesha uwezo mzuri kwa kucheza kwa kujihami zaidi na kufanya
mashambulizi ya kushitukiza, pia wameonekana kuimarika zaidi katika kucheza
mipira ya kona, na pasi ndefu na kwa jinsi hiyo wamekuwa wakipata mabao yao. Naye
Kocha wa Barca Tito Villanova kwa upande wake ameipongeza Celtic kwa ushindi
huo ingawa ametofautiana mshambuliaji wake kwa kusema kwamba hana la kuwalaumu
wachezaji wake kwa yaliyotokea katika mchezo huo. Villanova anakiri kuwa waliusoma
mchezo na walikuwa wakijua nini wanafanya na kuwawezesha kutengeneza nafasi
nyingi ingiwa hawakumalizia vizuri. Villanova amemsifu kipa wa Celtic kwa
kuokoa mipira ya hatari ya wachezaji wake huku akisema ingawa hapendi kufungwa
lakini hakukuwa na la ziada na hivyo amyakubalia matokeo hayo.
Kwa matokeo hayo Barcelona bado
inaendelea kushilia uongozi wa kundi hilo (kundi G) huku Celtic ikipaa hadi
nafasi ya pili juu Benfica na Spartak Moscoc.
Habari na picha kwa mujibu wa ESPN

Kichapo noma
ReplyDelete