 |
| Rais wa CAF: Issa Hayatou |
Rais wa shirikisho la soka la barani Africa (CUF) Issa Hayatou aukubali
mwaliko wa shirikisho la soka la Uganda (FUFA) na CECAFA kwenda nchini Uganda.
Kwa mujibu wa taarifa ya shirikisho la soka la Uganda Hayatou anategemewa
kuwasili nchini humo tarehe 22 Novemba (Alhamisi) majira ya jioni kufuatia
mwaliko maalum aliopokea toka kwa rais wa shirikisho la soka la Uganda Lawrence
Mulindwa na rais wa CECAFA Eng. Leodgar Tenga.
 |
Rais wa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo nduguCostant Omari Seleman |
 |
| Katibu Mkuu wa CAF Hicham El Amrani |
 |
| Makamu wa Rais CAF: Mohamed Raouraoua |
Katika ziara hiyo Hayatou atafuatana na maofisa mbalimbali wa CAF.
Miongoni mwa atakaombatana nao ni Katibu Mkuu wa CAF Hicham El Amran wengine
waliothibitisha ni Mohamed Raouraoua, Costant Omari na Ngangue Appolinaire.
Mara tu baada ya kuwasili na msafara wake anatazamiwa kukutana na Watendaji wa
FUFA jijini Kampala. Ijumaa tarehe 23
Novemba, atahudhuria CECAFA Congress katika hoteli ya Serena. Hayatou
anatazamiwa kuwa kusimamia ufunguzi rasmi wa CECAFA Tusker Cup katika uwanja wa Namboole siku ya jumamosi
tarehe 24, Novemba. Hayatou pia anatazamiwa kukutana na waziri wa michezo wa
Uganda Mheshimiwa Charles Bukalindi kwa mazungumzo mafupi.
No comments:
Post a Comment