Thursday, November 29, 2012

NADAL KUREJEA UWANJANI AUSTRALIAN OPEN


MANACOR, Hispania
Rafa Nadal Akijifua
Mchezaji nguli wa mchezo wa tennis Rafa Nadal wa Hispania ameanza kufanya mazoezi madogo madogo na kucheza uwanjani. Rafa ameonesha kupona na kuimarika kwa goti lake ambapo jumanne hii (jana) alianza mazoezi, hii ikiwa ni mara ya kwanza toka mwezi Agosti mwaka huu alipolazimika kujitoa kwenye michuano ya U.S. Open.

Nadal (26) amekuwa nje ya uwanja na hajashiriki mashindano yoyote yale tokea mwezi Juni mwaka huu alipotolewa na Czech Lukas Rosol katika raundi ya pili ya michuano ya Wimbledon. Rafa ambaye ni bingwa mara 11 wa gland slam kwa mchezaji mmoja mmoja ameanza mazoezi chini ya kocha wake ambaye pia ni ndugu wa baba yake Toni Nadal huko nyumbani kwao Manacor katika kisiwa cha Majorca. Pamoja na kuwa nje ya uwanja kwa kipindi chote hicho bado yupo katika nafasi ya nne (4) katika msimamamo wa wachezaji bora wa kiume duniani.

Rafa Nadal akisalimia Mashabiki
Rafa Nadal anatazamiwa kurejea kwenye michezo ya mashindano mwezi Januari mwakani wakati wa michuano ya Australian Open. Akiongea na shirika la habari la Uingereza (Reuters) alisema anajisikia vizuri na goti lake limeimarika vizuri na anafuraha kurudi uwanjani kwa mara nyingine baada ya miezi kadhaa. Anafurahia kujisikia tena nikicheza tennis kwa mara nyingine na vyema, kitakuwa ni kipindi kingine cha kupona kwangu, aliongeza.

Rafa Nadal Akiwa na moja ya vikombe vyake
Ameaza taratibu na anaendelea kila siku. Atajituma katika mazoezi ili arudi uwanjani na anategemea goti lake litapona kabisa hivi karibuni. Siku zote anatakiwa kuwa makini. Hasa akiwa amekaa kwa miezi kadhaa nje ya uwanja mwili unatakiwa uanze kuzoea kila kitu cha ndani ya uwanja na misuli nayo inatakiwa izoeshwe kwa taratibu zaidi Nadal aliongeza.

No comments:

Post a Comment