Saturday, December 1, 2012

Dumu Sports: MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL

Dumu Sports: MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL: Mesut Ozil katika moja ya mechi za timu yake ya Real Madrid MANCHESTER , Uingereza Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson atu...

MANCHESTER UNITED YAMWINDA MESUT OZIL

Mesut Ozil katika moja ya mechi za timu yake ya Real Madrid

MANCHESTER, Uingereza
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson atupia jicho lake kwa kiungo wa Real Madrid Mesut Ozil, 24. Mchezaji huyo raia wa Ujerumani amekuwa sio chaguo la kwanza la meneja wa Real Madrid Mreno Jose Maurinho tokea kuwasili kwa Luka Modric toka Tottenham Hotspurs ya Uingereza.

Mesut Ozil akiichezea ujerumani
katikaMashindano ya UEFA
Sir Alex Ferguson anamtaka Ozil kwa udi na uvumba aje kuchukua nafasi ya kiungo mkongwe wa timu hiyo Paul schools, 38. Kwa sasa Scholes anaonekana dhahiri kuchoka na huenda akatangaza kustaafu soka kwa mara ya pili mwishoni mwa msimu huu.

Kwa upande wa Ozil ameonekana hana furaha kwa kutokuwa chaguo la kwanza kwenye klabu yake. Mesut Ozil alijiunga na Real Madrid miaka miwili iliyopita akitokea timu ya Werder Bremen ya Ujerumani kwa ada ya pauni 12 milioni na amekuwa akipokea mshahara wa pauni 110,000 kwa wiki ambazo kwa timu kama Manchester United ni mshahara wa kawaida. Wataalam na wachambuzi wa soka wanatabiri kama Real Madrid itaamua kumuuza Ozil itamuuza kwa ada isiyopungua pauni 24 milioni.

Dumu Sports: LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL...

Dumu Sports: LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL...: Uingereza, Mshambuliaji wa timu ya Liverpool Luis Suarez ameshinda Barclays Golden Boot baada ya kuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufik...

LUIS SUAREZ ASHINDA BARCLAYS GOLDEN BOOT 10 - GOAL AWARD


Uingereza,
Mshambuliaji wa timu ya Liverpool Luis Suarez ameshinda Barclays Golden Boot baada ya kuwa mchezaji wa kwanza msimu huu kufikisha mabao kumi. Suarez amefikisha mabao hayo katika michezo 13 aliyoichezea timu yake ya Liverpool msimu huu.


Akiongea baada ya kupokea zawadi hiyo, Suarez alimshukuru meneja wake Brendan Rodgers kwa kumchochea kuongeza juhudi sio kwake yeye tu bali kwa kila mchezaji wa timu ya Liverpool. Pia alisema meneja wake anamchezesha kwa staili anayoipenda kwa kumfanya kuwa mshambuliaji huru na pekee kwenye kikosi sanjari na kumtia moyo kwamba atafunga mabao kitu ambacho kimemuongezea kujiamini.

Pia aliwapongeza viungo washambuliaji vijana wa timu hiyo Raheem Sterling na Suso kwa viwango vyao na jinsi wanavyojifunza toka kwa wachezaji wazoefu kama Steven Gerrard, Pepe Reina na Jamie Carragher na watakuja kufanikiwa sana siku za baadae.

Friday, November 30, 2012

Dumu Sports: MAVAZI YA MICHAEL JORDAN YACHAFUA HEWA KWENYE GOLF...

Dumu Sports: MAVAZI YA MICHAEL JORDAN YACHAFUA HEWA KWENYE GOLF...: California , Marekani Mavazi ya Michael Jordan yawa kituko kwenye viwanja vya mchezo wa golf. Tangu ajiunge na mchezo huo amekuwa akivaa...

MAVAZI YA MICHAEL JORDAN YACHAFUA HEWA KWENYE GOLF


California , Marekani
Mavazi ya Michael Jordan yawa kituko kwenye viwanja vya mchezo wa golf. Tangu ajiunge na mchezo huo amekuwa akivaa mavazi ambayo yanaonekana kuenda kinyume na utaratibu au utamaduni wa mavazi ya staha ya wachezaji wa mchezo huo


ADIOS HECTOR "MACHO" CAMACHO

Mama wa marehemu Hector "Macho" Camacho, Maria Matias
akilia "wamemuua, wamuuaa" wakati akitoa heshima ya mwisho 

SAN JUAN, Puerto Rico

Mabondia, wapenzi wa ngumi, na wanandugu wa bondia Hector “Macho” juzi (jumanne) kuuaga na kuuzika mwili wa mwanamasumbwi nguli. Waombolezaji waliobeba picha mbalimbali za Macho walipita mbele ya jeneza lake kumuaga marehemu.

waombolezaji wakitoa heshima za mwisho kwa marehemu
Hector "Macho" Camacho
Wakiongozwa na familia ya marehemu wakiongozwa na mama wa marehemu Maria Matia walitoa heshima za mwisho. Camacho aliuawa tarehe 20 Novemba akiwa kwenye maegesho ya magari ya bar moja katika mji wa Bayamon nchini Purto Rico. Katika tukio hilo rafiki yake wa karibu alifariki papo hapo na Camacho alifariki siku tatu baadaye akiwa kwenye matibabu.

Hadi sasa polisi nchini humo wanasema wana orodha ya washukiwa lakini bado hawajawatia mbaroni.

Thursday, November 29, 2012

NOVAK DJOKOVIC NA KUERTEN WAFUNGA KATIKA MECHI YA SOKA BRAZIL


RIO DE JANEIRO, Brazil

Novak Djokovic kulia akishangilia na Bebeto katikati na Edilson wa Brazil
Nyota wa mchezo wa tennis Novak Djokovic na bingwa mara tatu wa French Open Gustavo Kuerten walifunga katika mchezo wa kuchangisha fedha ulichezwa kabla ya mchezo wa ligi ya mpira wa miguu ya Brazil siku ya Jumapili tarehe 18 Novemba mwaka huu.

Kwa mujibu wa shirika la habari la Associated Press mchezo huo uliandaliwa na rafiki wa Djokovic , Mserbia mwenzake, Dejan Petkovic ambaye amekuwa akifuatilia michezo ya timu mbalimbali za Brazil kwa zaidi ya muongo mmoja. Katika mchezo huo wachezaji wa zamani wa timu ya taifa ya Brazili Zico na Bebeto walishiriki.

Novak Djokovic akishangilia na Bebeto wa Brazil 
Katika mchezo huo uliofanyika katika uwanja wa Engenhao ukitangulia mchezo wa Ubingwa wa Ligi ya Mpira wa Miguu ya Brazili kati ya Fluminense na Cruzeiro, uliishia kwa matokeo ya 3-3.

Dumu Sports: NADAL KUREJEA UWANJANI AUSTRALIAN OPEN

Dumu Sports: NADAL KUREJEA UWANJANI AUSTRALIAN OPEN: MANACOR , Hispania Rafa Nadal Akijifua Mchezaji nguli wa mchezo wa tennis Rafa Nadal wa Hispania ameanza kufanya mazoezi madogo mado...

NADAL KUREJEA UWANJANI AUSTRALIAN OPEN


MANACOR, Hispania
Rafa Nadal Akijifua
Mchezaji nguli wa mchezo wa tennis Rafa Nadal wa Hispania ameanza kufanya mazoezi madogo madogo na kucheza uwanjani. Rafa ameonesha kupona na kuimarika kwa goti lake ambapo jumanne hii (jana) alianza mazoezi, hii ikiwa ni mara ya kwanza toka mwezi Agosti mwaka huu alipolazimika kujitoa kwenye michuano ya U.S. Open.

Nadal (26) amekuwa nje ya uwanja na hajashiriki mashindano yoyote yale tokea mwezi Juni mwaka huu alipotolewa na Czech Lukas Rosol katika raundi ya pili ya michuano ya Wimbledon. Rafa ambaye ni bingwa mara 11 wa gland slam kwa mchezaji mmoja mmoja ameanza mazoezi chini ya kocha wake ambaye pia ni ndugu wa baba yake Toni Nadal huko nyumbani kwao Manacor katika kisiwa cha Majorca. Pamoja na kuwa nje ya uwanja kwa kipindi chote hicho bado yupo katika nafasi ya nne (4) katika msimamamo wa wachezaji bora wa kiume duniani.

Rafa Nadal akisalimia Mashabiki
Rafa Nadal anatazamiwa kurejea kwenye michezo ya mashindano mwezi Januari mwakani wakati wa michuano ya Australian Open. Akiongea na shirika la habari la Uingereza (Reuters) alisema anajisikia vizuri na goti lake limeimarika vizuri na anafuraha kurudi uwanjani kwa mara nyingine baada ya miezi kadhaa. Anafurahia kujisikia tena nikicheza tennis kwa mara nyingine na vyema, kitakuwa ni kipindi kingine cha kupona kwangu, aliongeza.

Rafa Nadal Akiwa na moja ya vikombe vyake
Ameaza taratibu na anaendelea kila siku. Atajituma katika mazoezi ili arudi uwanjani na anategemea goti lake litapona kabisa hivi karibuni. Siku zote anatakiwa kuwa makini. Hasa akiwa amekaa kwa miezi kadhaa nje ya uwanja mwili unatakiwa uanze kuzoea kila kitu cha ndani ya uwanja na misuli nayo inatakiwa izoeshwe kwa taratibu zaidi Nadal aliongeza.

Tuesday, November 27, 2012

Dumu Sports: RICKY HATTON ASTAAFU BAADA YA KUPIGWA TENA

Dumu Sports: RICKY HATTON ASTAAFU BAADA YA KUPIGWA TENA: Manchester Sir Richard 'Ricky' Hatton Bondia Mwingereza Ricky Hatton (34) ametangaza kustaafu tena kwa mara ya pili baada ya jaribio ...

RICKY HATTON ASTAAFU BAADA YA KUPIGWA TENA

Manchester
Sir Richard 'Ricky' Hatton

Bondia Mwingereza Ricky Hatton (34) ametangaza kustaafu tena kwa mara ya pili baada ya jaribio lake la kurudi tena kwenye masumbwi kushindwa. Katika pambano lake la kurudi kwenye mchezo huu aliambulia kichapo kikali alipopigwa kwa ‘knockout’ na Vyacheslav Senchenko wa Ukraini jijini Manchester Uingereza jumamosi iliyopita.

Mashabiki wapatao 20,000 walijitokeza kuja kushuhudia kurudi kwa bingwa huyo wa zamani wa dunia katika mji wake wa nyumbani. Ricky alianza pambano hilo vizuri lakini alionekana kuchoka kadri muda ulivyokuwa ukisonga mbele na kumpa nafasi Senchenko (35) kumtupia makonde makali. Ricky alilamba mchanga na alipohesabiwa alishindwa kuinuka na kumfanya mwamuzi kumpa ushindi Senchenko. Senchenko ameendelea kuboresha rekodi yake ambapo hadi sasa amepoteza pambano moja (1)tu kati ya thelasini na nne (34) aliyocheza.
Sir Richard Hatton  akionesha moja ya mikanda yake

Sir Richard 'Ricky' Hatton akiaga mashabiki alipotangaza kustaafu kwa mara ya pili
Akiongea baada ya pambano Hatton alisema"nilitaka walau pambano moja zaidi kuona kama naweza kurejea, na nimeona sintoweza, nimeona sina uwezo tena.” "Nimejiangalia kwenye kioo na nikajiambia mwenyewe nimejitahidi, na sijilaumu”.

Monday, November 26, 2012

Dumu Sports: REKODI BORA KWA MABONDIA CHINI YA MIAKA 25

Dumu Sports: REKODI BORA KWA MABONDIA CHINI YA MIAKA 25: 1.    Adrien Broner (25-0, 21 KOs), Age: 23 2.    Saul Alvarez (41-0-1, 30 KOs), Age: 22 3.    Danny Garcia (25-0, 16 KOs), Age: 24 ...

'MACHO' CAMACHO AFARIKI DUNIA


SAN JUAN, Puerto Rico
Hector 'Macho' Camacho katikati akiwa na warembo
Amy Camacho mke wa Hector 'Macho' Camacho
Hector ''Macho'' Camacho katika uhai wake alikuwa ni bondia anayejituma na kujiamini mwenye ngumi nzito na mtindo wa kujituma katika mapambano yake na mtukutu nje ya uwanja. Hector ‘Macho’ Camacho alikutwa amefariki siku ya jumamosi baada ya kuvamiwa katika sehemu ya kuegeshea magari katika mji wa Bayamon huko Puerto Rico ambako ndiko alikozaliwa. Polisi walikuta pakti za madawa ya kulevya aina ya cocaine katika gari alilokuwemo.
Camacho, amefariki akiwa na umri wa miaka 50, atakumbukwa kwa uwezo wake mkubwa wa kuburudisha na kupendwa na mashabiki ambapo walikuwa wakimpokea kwa kibwagizo ''It's Macho time!'' kabla hajapanda ulingoni. Camacho alikuwa na kipaji na mbinu zilizowatisha na wapinzani wake na kumfanya kuwa bondia wa kiwango cha juu katika kipindi hicho.
Enzi za ujana wake

Macho akipelekwa hospitali
Macho alipigana kwa kipindi cha miongo mitatu tokaea pambano lake la kwanza dhidi ya David Brown jijini New York mwaka 1980 hadi pambano lake dhidi ya Saul Duran huko Kissimmee, Florida, mwaka 2010. Katika uhai wake alipambana na mabondia nyota mbalimbali wakiwamo Sugar Ray Leonard, Felix Trinidad, Oscar De La Hoya, Roberto Duran na wengineo wengi.

HII NI KITU NYINGINE

Kulia ni kabla na kushoto ni baada ya pambano
Andre Berto akiwa mazoezini
Anavyoonekana Andre Berto mara baada ya kupata kichapo kitakatifu toka kwa Robert Guerrero katika pambano la raudi 12 usiku wa kuamkia jumamosi. Bingwa huyo wa dunia wa zamani wa ‘Welterweight’ alipigwa kwa pointi 116-110 

Acky: Msanii wa filamu nchini Tanzania John Stephano Mag...

Acky: Msanii wa filamu nchini Tanzania John Stephano Mag...:   HABARI: Msanii wa filamu nchini Tanzania John Stephano Maganga afariki dunia katika hospital ya Muhimbili kutokana na Ugonjwa wa ...

REKODI BORA KWA MABONDIA CHINI YA MIAKA 25


1.   Adrien Broner (25-0, 21 KOs), Age: 23
2.   Saul Alvarez (41-0-1, 30 KOs), Age: 22
3.   Danny Garcia (25-0, 16 KOs), Age: 24
4.   Tyson Fury (19-0, 14 KOs), Age: 24
5.   Leo Santa Cruz (22-0-1, 13 KOs), Age: 24
6.   Miguel Angel Garcia (30-0, 26 KOs), Age: 24
7.   George Groves (15-0, 12 KOs), Age: 24
8.   Javier Fortuna (20-0, 15 KOs), Age: 23
9.   Kazuto Ioka (10-0, 6 KOs), Age: 23
10.              Thomas Oosthuizen (21-0-1, 13 KOs), Age: 24

Thursday, November 22, 2012

hujuma- Yanga football fan cries (Remix)

Machozi ya Shabiki wa Yanga

mzungu wa simba sports club akimvua nguo za njano jamaa wa yanga

BEN ARFA, MESSI, NEYMAR, NA FALCAO KUCHUANA FIFA PUSKAS 2012

Shirikisho la soka la Dunia FIFA limetangaza majina ya wachezaji kumi wanaowania tuzo ya mfungaji wa goli bora FIFA Puskas kwa mwaka 2012. Jumla ya magoli 10 yameteuliwa na kura zimeanza kupigwa ambapo zitapigwa hadi tarehe 29 Novemba 2012 ambapo yatapunguzwa na kubaki matatu.
Goli bola liatatangazwa Januari 7 2013 wakati wa ugawaji wa tuzo ya mchezaji bora wa FIFA (FIFA Ballon d’Or 2012) jiji Zurich. Jina la Puskas limetokana na mchezaji nguli wa Hungary Ferenc Puskas.
Magoli yaliyochaguliwa ni:
1.   Hatem Ben Arfa: (Newcastle v Blackburn Rovers, 07 Januari 12)
2.   Gaston Mealla: (Nacional Patosi v The Strongest, 29 Januari 12)
3.   Agyemang Badu: (Ghana v Guinea 01 Februari 12)
4.   Miroslav Stoch: (Fenerbahce v Gencelerbirligi, 03 Machi 12)
5.   Neymar: (Santos v Internacional, 07 Machi 12)
6.   Moussa Sow: (Fenerbahce v Galatasaray, 17 Machi 12)
7.   Eric Hassli: (Vancouver Whitecaps v Toronto FC, 16 May 12)
8.   Radamel Falcao: (America de Cali v Atletico Madrid, 19 May 12)
9.   Lionel Messi: (Brazil v Argentina, 09 June 12)
10.               Olivia Jimnez: (Mexico v Switzerland, 22 Agosti 12)
Yatazame magoli hayo na upige kula katika link ifuatayo:

Dumu Sports: MATOKEO YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE WIKI HII

Dumu Sports: MATOKEO YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE WIKI HII: Jumatano, 21 Novemba 2012 Dynamo Kiev 0-2 Paris Saint-Germain FC porto 3-0 Dinamo Zagreb Arsenal 2-0 Mo...

MATOKEO YA UEFA CHAMPIONS LEAGUE WIKI HII
















Jumatano, 21 Novemba 2012
Dynamo Kiev 0-2 Paris Saint-Germain
FC porto 3-0 Dinamo Zagreb
Arsenal 2-0 Montpellier
Schalke 04  1-0 Olympiakos
Zenit St Petersburg 2-2 Malaga
Anderlecht 1-3 AC Milan
Ajax Amsterdam 1-4 Borussia Dortmund
Manchester City 1-1 Real Madrid

Jumanne, 20 Novemba 2012
FC Nordsjaelland 2-5 Shakhtar Donetsk
Juventus 3-0 Chelsea
BATE Borisov 0-2 Lille
Vallencia 1-1 Bayern Munich
Spartak Moscow 0-3 Barcelona
Benfica 2-1 Celtic
CFR Cluj-Napoca 3-1 Braga
Galatasaray 1-0 Machester United 

Dumu Sports: MAN CITY YALAMBA MCHANGA

Dumu Sports: MAN CITY YALAMBA MCHANGA: Kocha wa Man City Roberto Mancini Mabingwa wa Uingereza Manchester City jana waliaga rasmi michuano ya klabu bingwa barani ulaya kwa m...

MAN CITY YALAMBA MCHANGA

Kocha wa Man City Roberto Mancini

Mabingwa wa Uingereza Manchester City jana waliaga rasmi michuano ya klabu bingwa barani ulaya kwa mara ya pili mfululizo. Bao la mapema la Mfaransa Karima Benzema aliloifungia timu yake ya Real Madrid ya Hispania liliweza kuikatisha ndoto ya Man City kuingia hatua ya 16 bora ya michuano hiyo. Katika mchezo huo timu hizo zilitoka sare ya bao 1-1 bao lakusawazisha la Man City likifungwa Sergio Kun Aguero kwa njia ya penati dakika 15 kabla ya mchezo kumalizika baada ya kufanyiwa madhambi ndani ya eneo la hatari na Alvaro Alberoa ambaye alitolewa kwa kadi nyekundu.
Kocha wa Arsenal Arsene Wenger

Wakati huo huo Arsenal ilikata tiketi yake kwenye hatua ya 16 bora baada ya kuwafunga mabingwa wa Ufaransa Montpellier kwa mabao 2-0. Mabao hayo yalifungwa na Jack wilshere na Lukas Podolski.

ROBERTO DI MATTEO APIGWA CHINI

Roberto Di Matteo akifuatilia moja ya
michezo alipokuwa kocha wa Chelsea

Chelsea imetangaza kumtema maeneja wake Mtaliano Roberto Di Matteo kwa kilichoelezwa kutokuonesha mwenendo mzuri wa timu. Di Matteo mabaye katika uongozi wake klabuni hapo aliingoza Chelsea maarufu kama “The Blues”michezo 42 ambapo ilishinda 24, kupoteza 9 na kutoka sare 9. Kufutwa kazi kwa Di Matteo's kulitazamiwa kufuatia klabu hiyo ya London kupoteza kwa mabao 3-0 dhidi ya Juventus na kuifanya kuwa bingwa mtetezi wa kwanza kutolewa katika hatua ya makundi katika historia ya mashindano ya klabu bingwa barani ulaya (UEFA Champions League).
Kwa mujibu wa taarifa iliyotelewa na mtandao wa klabu www.chelseafc.com, klabu hiyo yenye uwanja wake Stanford Bridge imethibitisha kuondoka kwa Di Matteo. Sehemu ya taarifa ilisema Chelsea imevunja mkataba na na meneja Roberto Di Matteo. Kiwango cha mchezo na matokeo ya timu kwa siku za karibuni yamekuwa hayaridhishi na mmiliki na bodi wameona mabadiliko ni lazima yafanyike sasa kuiwezesha klabu kuelekea kwenye mwelekeo sahihi kwa kuwa ikielekea kwenye kipindi muhimu zaidi cha msimu.
Roberto Di Matteo akisherehekea ubingwa wa UEFA
Champions League na wapenzi wa Chelsea jijini London

Klabu hiyo ilikumbana na wakati mgumu wakati ikitafuta nafasi ya kuingia katika hatua ya makundi za ligi ya mabingwa huku ikiendelea kupigana kubakia katika nafasi za juu katika ligi ya nyumbani. Lengo la klabu ni kubakia katika nafasi ya kiushandani zaidi katika mashindano yote ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Roberto Di Matteo alipokuwa mchezaji wa Chelsea
Pia klabu hiyo imemshukuru meneja huyokwa yote mazuri aliyoifanyia klabu hiyo kubwa hasa likiwa ni kuiwezesha kuchukua ubingwa katika ligi ya klabu bingwa barani ulaya sanjari na kuipa ushindi wa kombe la chama cha soka cha Uingereza (FA Cup). Klabu hiyo inasema haitaweza kumsahau Muitaliano huyo kwa mchango wake mkubwa alioutoa ambao ni wa kihistoria katika klabu hiyo na imesema iko tayari kumkaribisha muda wowote ule.
Wakati huohuo klabu hiyo ikitazamiwa  kumtangaza kocha mpya wa klabu hiyo baada ya kumfukuza kazi Di Matteo, kumekuwa na kundi linalomlaumu Di Matteo kwa matokeo mabaya katika michezo ya hivi karibuni. Katika michezo nane ya mwisho aliwaongoza wazee wa ‘darajani’ kushinda michezo ,miwili tu kitu kilichomplekea mmiliki wa klabu hiyo asiye mvumilivu Roman Abramovich kumfukuza kazi.

Monday, November 19, 2012

MUSONYE ATANGAZA MAJINA YA MAREFA CHALLENGE

Katibu Mkuu wa CECAFA: Nicholas Musonye

Rais CECAFA: Lodgar Tenga

Katibu mkuu wa CECAFA Nicholas Musonye ametangaza majina ya waamuzi watakaochezesha Tusker Senior Challenge Cup 16 ambao 8 kati yao ni waamuzi wa wasaidizi. Wamuzi hao wanatazamiwa kupima afya zao ijumaa tarehe 23 chini ya usimamizi wa mwamuzi anayetambuliwa na Shirikisho la Soka Duniani FIFA Charles Masembwe.
 

Majina ya waamuzi walichaguliwa na nchi wanazotoka kwenye mabano ni kama ifuatavyo:


Waamuzi:
 
Thierry Nkurunzinza (Burundi), Maeruf Mensur (Eritrea), Antony Ogwayo (Kenya),Hakizimana Louis (Rwanda), Ali Kalyango (Uganda), Mohamed Hussein El Fadhil (Sudan), Denis Batte (Uganda) and Israel Mujuni (Tanzania).

Waamuzi Wasaidizi:

Mark Ssonko (Uganda), Mussie Kinde (Ethiopia), Peter Sabatia (Kenya), Idam Mohammed (Sudan), Hakizimana Ambroise (Rwanda), Kinduli Ali (Zanzibar), Clemence Erasmo (Tanzania) and Omar Abukar (Somalia).

Dumu Sports: HAYATOU KUTUA UGANDA

Dumu Sports: HAYATOU KUTUA UGANDA: Rais wa CAF: Issa Hayatou Rais wa shirikisho la soka la barani Africa (CUF) Issa Hayatou aukubali mwaliko wa shirikisho la soka la Uga...

HAYATOU KUTUA UGANDA

Rais wa CAF: Issa Hayatou
Rais wa shirikisho la soka la barani Africa (CUF) Issa Hayatou aukubali mwaliko wa shirikisho la soka la Uganda (FUFA) na CECAFA kwenda nchini Uganda. Kwa mujibu wa taarifa ya shirikisho la soka la Uganda Hayatou anategemewa kuwasili nchini humo tarehe 22 Novemba (Alhamisi) majira ya jioni kufuatia mwaliko maalum aliopokea toka kwa rais wa shirikisho la soka la Uganda Lawrence Mulindwa na rais wa CECAFA Eng. Leodgar Tenga.

Rais wa Shirikisho la Soka la Jamhuri ya
 Kidemokrasia ya Congo nduguCostant Omari Seleman
Katibu Mkuu wa CAF Hicham El Amrani
Makamu wa Rais CAF: Mohamed Raouraoua 
Katika ziara hiyo Hayatou atafuatana na maofisa mbalimbali wa CAF. Miongoni mwa atakaombatana nao ni Katibu Mkuu wa CAF Hicham El Amran wengine waliothibitisha ni Mohamed Raouraoua, Costant Omari na Ngangue Appolinaire. Mara tu baada ya kuwasili na msafara wake anatazamiwa kukutana na Watendaji wa FUFA jijini  Kampala. Ijumaa tarehe 23 Novemba, atahudhuria CECAFA Congress katika hoteli ya Serena. Hayatou anatazamiwa kuwa kusimamia ufunguzi rasmi wa CECAFA Tusker Cup  katika uwanja wa Namboole siku ya jumamosi tarehe 24, Novemba. Hayatou pia anatazamiwa kukutana na waziri wa michezo wa Uganda Mheshimiwa Charles Bukalindi kwa mazungumzo mafupi.

Wednesday, November 14, 2012

LEON OSMAN: SIJAKATA TAMAA KUCHEZEA ENGLAND

Leon Osman

Kiungo wa Everton anayemalizia mpira wake na kuonekana kuelekea ukingoni mwa kipaji chake Leon Osman (31) amesema hajakata tamaa na hatakata tamaa. Osman anategemea kucheza mchezo wake wa kwanza wa kimataifa baada ya kuitwa kwa mara ya kwanza na kocha wa Uingereza Roy Hogson.

Leon Osman katika moja ya mechi za watani wa jadi (Derby Match) dhidi ya 
Liverpool
England baadae leo itapambana na Sweden katika mchezo wa kirafiki unaotambuliwa na FIFA utakaofanyika jijini Stockholm, Sweden. Leon Osman amejumuishwa kwenye kikosi cha England kilichoenda Stockholm.

Harambee Stars Yatua Mwanza

Kocha mkuu wa Taifa Stars Kim Paulsen

Harambee Stars ya Kenya jana iliwasili katika uwanja wa ndege wa Mwanza tayari kwa mchezo wake wa leo dhidi ya Taifa Stars. Kocha mkuu wa Wakenya hao Henri Michel amejinadi kuwa atatumia kikosi kilekile kilichoisumbua Afrika Kusini katika mchezo wa kirafiki uliochezwa Oktoba 16 katika uwanja wa Nyayo. Katika mchezo huo Afrika Kusini ilipata ushindi mwembamba wa mabao 2-1.

Harambee Stars imewasili bila ya kipa wake namba moja Arnold Origi aneyekipiga katika timu ya Ullkisa amabaye amebanwa na ratiba ngumu ya ligi. Pia Wakenya hao watamkosa mshambuliaji wao hatari Victor Wanyama ambaye anakabiliwa na majeruhi. Michel amemuita Jactone Odhiambo wa Ulinzi kuziba pengo la Origin a Anthony Akumu wa Gor Mahia kuziba pengo la Wanyama.

Naye kocha wa Taifa Stars Kim Paulsen amefanya mabadiliko kidogo kwenye kikosi chake kwa kuwaacha Said Bahanuzi (Yanga) na Haruna Moshi “Boban” (Simba). Paulsen ameongeza kiungo hatari Amri Kiemba (Simba) pamoja na damu changa kama Frank Domayo (Yanga), Simon Msuva (Yanga), Christopher Edward (Simba). Pia katika kikosi hicho hakuwaacha wachezaji wenye asili ya visiwani ambao wataruhusiwa kujiunga na Zanzibar Heroes mara tu baada ya mchezo wa Leo. Wachezaji hao ni Aggrey Morris, Said Nassor “Cholo”, na Issa Rashid.

THE CRANES KUIVAA HARAMBEE STARS

Timu ya taifa ya Kenya "Harambee Stars"

Timu ya soka ya Uganda The Cranes itashuka dimbani kuikaribisha timu ya taifa ya Kenya almaarufu Harambee Stars. Timu hizi zitachuana katika mchezo wa ufunguzi wa michuano ya CECAFA Challenge Cup mchezo utakaochezwa tarehe 24 Novemba mwaka huu jijini Kampala.

Timu ya taifa ya Uganda "The Cranes"
The cranes bado wana uchungu wa kubaniwa na Harambee Stars nafasi ya kushiriki michuano ya mataifa ya Afrika. Katika mchezo huo Wakenya hao waliilazimisha The Cranes sare isiyo na magoli (suluhu), mchezo huo ulifanyika huko Namboole. The Cranes pia katika mchezo wake wa mwisho ilifungwa kwa penati 8-9 na Zambia hapohapo Namboole mwezi Januari mwaka huu.

Kabla ya mechi hiyo ya ufunguzi timu za Ethiopia na Sudani Kusini zitapambana katika mchezo unaotazamiwa kuanza majiara ya saa tisa (9) alasiri kwa saa za Afrika Mashariki. Kwa sasa Uganda ipo katika nafasi ya 88 na Kenya ipo katika nafasi ya 130 ya ubora wa viwango vya soka duniani.

Tuesday, November 13, 2012

STARS KUKIPIGA NA HARAMBEE STARS

Kikosi cha Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars), Picha kwa hisani ya tff.or,tz

Timu ya Taifa ya mpira wa miguu Taifa Stars inatazamia kushuka katika dimba la CCM Kirumba jijini Mwanza kesho jumatano tarehe 14 itakapo wakaribisha Harambee Stars ya Kenya. Taifa Stars na Harambee Stars zitakwaana katika mchezo wa kirafiki unaotambuliwa na Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

Kwa mujibu wa mtandao wa Shirikisho la Vyama vya Mpira wa Miguu Tanzania tff.or.tz, mchezo huo unatazamiwa kuanza majira ya saa 10 jioni. Mchezo huu ni muhimu kwa timu zote mbili, ambapo kwa upande wa Kenya itakuwa ikijipima nguvu kujiandaa na mchezo wa hatua ya makundi wa kuwania nafasi ya kushiriki kombe la dunia na pia kama ilivyo kwa Taifa Stars pia mchezo huo ni maandalizi ya michuano ya kombe la CECAFA Challenge.

Taifa Stars kwa sasa ipo katika nafasi ya 134 katika viwango vya soka duniani, itaingia dimbani kuchuana na Kenya iliyo katika nafasi ya 130. Mbali na maandalizi ya CECAFA Challenge Cup, mchezo huo ni muhimu kwa Stars inayopigana  kurejea katika kiwango chake juu, ambapo katika historia ni nafasi ya 65 ambayo ilifikiwa mnamo mwaka 1965.

Friday, November 9, 2012

Wenger Alegeza Msimamamo Wake

Jack Wilshere
Meneja wa washika bunduki wa London Mfaransa Arsene Wenger amelegeza msimamo wake na kumrushusu mchezejai wake Jack Wilshere (20) kuchezea timu ya taifa ya Uingereza itakapopambana na Sweden wiki ijayo. Awali Wenger alimtaka kocha wa Uingereza Roy Hogson kumpumzisha mchezaji huyo kwa kuwa alikuwa majeruhi kwa muda mrefu. Mameneja hao walifikia muafaka wa kumruhusu Wilshere mara baada ya mchezo kati ya Arsenal na Manchester United ambapo Wilshere alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Akiongea na skysports.com Wenger alisema "Ninaona ni mapema mno kwa Jack lakini nimeongea na Roy Hodgson kwa simu na tumeelewana na kufikia muafaka mzuri”
 "Kizuri zaidi ni kuwa hatacheza mwishoni mwa wiki hii kwa kuwa na adhabu ya kadi nyekundu hivyo atapumzika na kujiunga na kikosi kama Roy anavyotaka”